Somo: MAJIRA NA NYAKATI ZIMEBEBA MAISHA YAKO. (Part 16: MWAMUZI WA MWIS...
Somo: MAJIRA NA NYAKATI ZIMEBEBA MAISHA YAKO
°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°
Fuatilia YouTube.
Https://youtube.com/@Rwizakakiza
Sehemu 16:
""Kwa KILA JAMBO kuna MAJIRA yake, Na WAKATI kwa KILA KUSUDI chini ya mbingu""
.....Mhubiri 3:1.....
6. AINA 2 ZA MAJIRA NA NYAKATI KATIKA MAISHA YAKO.
6. 2. MAJIRA NA NYAKATI ZA MUNGU
Haya ni majira na nyakati ambazo mwamuzi wa mwisho ni MUNGU ingawa hata kama mwanadamu atashirikishwa na MUNGU bado maamuzi ya mwisho ni ya MUNGU mwenyewe.
Mwamuzi wa mwisho kwenye majira na nyakati ni MUNGU pekee. Hata kama giza au watu au mamlaka au adui amekuamria Mabaya yaje juu yako, LAKINI YUPO MUNGU MWAMUZI WA MWISHO ANASEMA....
(i). HAUTAKUFA BALI UTAISHI.
MUNGU hataki mtu yeyote afe kabla ya majira na nyakati zake, maana akifa kabla ya wakati wake, kuna makusudi ya MUNGU hayatimiza, hutakuwa na kusimulia, Tambua majira na nyakati za MUNGU kwenye maisha yako. Yupo Roho Mtakatifu afunuaye mambo yajayo, ana uwezo wa kukwambia lini utaondoka, ukiwa na uhakika huo hata kama Ikitokea leo mtu anakwambia utakufa, Wewe kwa uhakika utamwambia.....
......Sitakufa bali nitaishi, Nami nitayasimulia matendo ya BWANA.
.....Zaburi 118:17.....
(ii). HAUTAKUWA TASA BALI UTAZAA WATOTO.
Ni kweli wewe ni tasa kwa kila kitu hakuna unachozalisha iwe ni mali au vitu au watoto hata ukizalisha vinakufa. Lakini yapo majira na nyakati za MUNGU ambazo ndio leo, MUNGU anasema hivi...
.....Hapatakuwa na mwenye KUHARIBU MIMBA , wala ALIYE TASA, katika nchi yako; na hesabu ya siku zako NITAITIMIZA.
.......Kutoka 23:26......
Ni Ahadi ya MUNGU ujenge nyumba Ukae ndani yake, Na ndani ya nyumba uwe na Uzalishaji na kula matunda ya uzalishaji wako, ambaye hujaoa au kuolewa chukua hatua ya imani. Leo ni wakati wako wa kudai haki yako majira na nyakati za MUNGU kwako zimefika, MUNGU anasema......
......JENGENI nyumba, MKAKAE ndani yake, KAPANDENI bustani, MKALE MATUNDA yake; OENI wake, MKAZAE wana na binti; KAWAOZENI wake wana wenu, mkawaoze waume binti zenu, WAZAE wana na binti; MKAONGEZEKE huko wala MSIPUNGUE.
......Yeremia 29:5-6.....
(iii). HAUTAKUWA MASKINI, BALI TAJIRI.
Ni kweli ulizaliwa kwenye umaskini mpaka sasa wewe ni maskini lakini haimaanishi utaendelea kuwa maskini. Ongeza bidii katika kutenda kazi iliyo halali na huku ukikumbuka Neno hili kwamba....
.......Umejua neema ya BWANA wetu YESU KRISTO, jinsi alivyokuwa MASKINI kwa ajili yako, ingawa alikuwa TAJIRI, ili kwamba WEWE UPATE kuwa TAJIRI kwa umaskini wake.
.......2 Korintho 8:9.......
Unavyoendelea kujibidiisha katika utendaji MUNGU anaachilia NGUVU YA UTAJIRI ndani yako, Sasa ni nyakati na Majira ya kuaga umaskini umefika Ongeza bidii, ila usimsahau BWANA YESU.
.......Hapo usiseme moyoni mwako, NGUVU ZANGU na UWEZO wa MKONO wangu ndio ULIONIPATIA UTAJIRI huo. Bali utamkumbuka BWANA, MUNGU wako, maana NDIYE akupaye NGUVU za KUPATA UTAJIRI; ili alifanye imara AGANO lake alilowapa baba zako, kama hivi leo.
......Kum 8:17-18.....
(iv). SITAKUACHA KAMWE.
Ni kweli umeachwa, unateseka, unanyanyaswa na umetengwa mpaka unaona dunia imekuacha na MUNGU hakukumbuki, Yote hayo yalikuwa ni majira na nyakati tu, kuanzia leo ni wakati wako wa kukumbuka hata na wale waliokusahau na MUNGU Hawezi kukuacha na hatakuacha kamwe nawe usimwache upo kiganjani mwake.
.....Wewe umesema, "YEHOVA AMENIACHA, BWANA AMENISAHAU. Je! Mwanamke aweza kumsahau mtoto wake anyonyaye, hata asimhurumie mwana wa tumbo lake? Naam, HAWA WAWEZA KUSAHAU, lakini MIMI SITAKUSAHAU WEWE. Tazama, NIMEKUCHORA katika vitanga vya mikono yangu; kuta zako ziko mbele zangu daima.
......Isaya 49:14-16......
(v). NJOO ULIVYO NA DHAMBI ZAKO.
Ni ukweli usiopingika kwamba wewe ni mdhambi na watu wote tunajua wewe ni mdhambi na MUNGU anajua wewe ni mdhambi, Lakini leo majira na wakati wa MUNGU umefika, MUNGU anakuita njoo....
.....Haya, njoni, tusemezane, asema BWANA. Dhambi zako zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu. Kama UKIKUBALI na KUTII leo utakula mema ya nchi".
......Isaya 1:18-19.....
Sisi tumekuona huwezi kusamehewa lakini kumbuka mwamuzi wa mwisho ni MUNGU, leo ni majira na wakati wa MUNGU kwa ajili yako kubadilika ili kuishi na MUNGU upya.
(vi). WEWE NI WATHAMANI, NA MWENYE HESHIMA.
Ni kweli umekosa heshima, huthaminiwi, hupendwi na hukumbukwi tena. Lakini haimaanishi MUNGU hakuoendi. MUNGU anakupenda sana sana kwa sababu wewe ni wa THAMANI kubwa kwake na mwenye heshima kubwa kwa MUNGU. Ni majira na nyakati za MUNGU kutambulisha heshima na thamani yako kwa ulimwengu maana anakupenda, nawe jipende na ujithamini na kujiheshimu.
......Kwa kuwa wewe ni wa THAMANI machoni pangu, na mwenye KUHESHIMIWA , nami NIMEKUPENDA; kwa sababu hiyo NITATOA watu kwa ajili yako; na kabila za watu kwa ajili ya maisha yako.
......Isaya 43:4....
(vii). ULIYECHOKA NA KUKATA TAMAA NJOO.
Maisha yamekuchosha, watu wamekuchosha, kazi imekuchosha, Huduma imekuchosha, familia imekuchosha, maneno yamekuchosha, Magonjwa, taabu na mateso vimekuchosha na kadhalika, Ni kweli umechoka na umekata tamaa. Leo Neno moja tu la YESU mtwike hayo yote yalikuchosha na YESU atakupumzisha ili upate raha nafsini mwako. BWANA YESU anasema hivi....
.......Njoni kwangu, ninyi nyote MSUMBUKAO na wenye KULEMEWA na MIZIGO, nami NITAWAPUMZISHA. Jitieni NIRA yangu, MJIFUNZE kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi MTAPATA RAHA NAFSINI mwenu".
...... Mathayo 11:28-29.....
(viii). MWENYE AIBU, WEWE NI JASIRI NA HODARI.
Kuna mambo ukiyatazama unaona aibu inakujia, Mengine ukiyasema ni aibu, imekuwa ni siri yako mwenyewe lakini yamegeuka kuwa mateso kwa sasa. Mwingine hadhi yako uliyonayo na kufanya kitu cha kawaida unaona ni aibu, Umefirisika unawaza watu watanionaje watanicheka. Wengine ni aibu ya kuachwa, kusimama mbele za watu, nk. Umekuwa mtumwa wa aibu kumbuka YESU aliidharau aibu, akajivika ujasiri na Uhodari akashinda. Ni majira na nyakati za MUNGU kuondolewa aibu yako, kubali na chukua hatua uwe shujaa, aibu itakufedhehesha kwa muda lakini utapata heshima ya kudumu.
.......Tukimtazama YESU, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya FURAHA iliyowekwa mbele yake ALIUSTAHIMILI MSALABA na KUIDHARAHU AIBU, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha MUNGU.
.....Ebrania 12:2....
(ix). ULIYESHINDWA, INUKA ANZA UPYA.
Naongea na wewe uliyekata tamaa kwa sababu UMESHINDWA kufikia malengo yako. Kila ukipanga unashinwa, kila mipango haikamiliki, masomo umeishia katikati, Biashara ni hasara unatamani uachane nayo, Mahusiano unaona hayana mwelekeo, mwenzi wako humwelewi unatamani mwachane. Majira na wakati wa MUNGU umefika inuka tena upya mara pili ule (Neno la MUNGU la leo hii) songa mbele mpaka ufike kwenye mafanikio yako (mlima Horebu) yapo mema mbele usikate tamaa.
......Malaika wa BWANA akamwendea mara ya pili, akamgusa, akasema, INUKA, ULE; maana SAFARI hii ni KUBWA MNO kwako. Akainuka, akala, akanywa, AKAENDA katika NGUVU za CHAKULA hicho siku arobaini mchana na usiku hata akafika Horebu, mlima wa MUNGU.
.....1Falme 19:7-8.....
(x). USIOGOPE.
Kuweza kutimiza vyema majira na nyakati za MUNGU ONDOA HOFU ya kesho yako. (iwe ni kifo, Magonjwa, madeni, vitisho, mateso, aibu, kufeli, kuzomewa, kuachwa, nk), usiogope shikamana na MUNGU mwenye hatima na maamuzi ya mwisho kwenye maisha yako yote.
.....USIOGOPE, kwa maana Mimi MUNGU ni pamoja nawe; USIFADHAIKE, kwa maana mimi ni MUNGU wako; NITAKUTIA NGUVU, naam, NITAKUSAIDIA, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu".
.....Isaya 41:10.....
Ni swala la majira na wakati wa MUNGU tu, Wewe sio wa kawaida, Yupo mwaamuzi wa mwisho, MUNGU ambaye hashindwi na chochote, ndiye mwenye hatima yako, mwamini YESU ili kitu au mwanadamu yeyote asikupangie hatima yako, usipomwamini YESU KRISTO mwenye hatima ya maisha yako, utapangiwa majira na nyakati za kuishi.
Hitimisho.
....Tutaendelea....
Rejea
“Indeed, I have inscribed [a picture of] you on the palms of My hands; Your city walls [Zion] are continually before Me".
.......Isaiah 49:16.......
Ev. Erasmus Pascrates Kakiza
+255 782 546 914
@2024 The year of my shining.
0 notes